Tuesday, July 5, 2016

 Julius Mtatiro: Kwa Uwazi Kabisa Nasema Hii ni AIBU KUU Kwa Taifa la Tanzania
Tunatangaziwa kwa mbwembwe kuwa Taifa letu linaenda kujifunza Teknolojia kutoka Rwanda. So shameful! Taifa ambalo limeshiriki kupigania uhuru wa nchi karibia zote za Afrika. Taifa lenye mamia ya MAPROFESA na wataalamu wa Teknolojia za kila namna. Kwa hiyo hawa MAPROFESA wetu tunaowalipa mamilioni ya mishahara kwa mwezi, tena waliosomea teknolojia mbalimbali Uchina, Urusi, Marekani, Ujerumani, Uingereza na kwingineko (kwenye vyuo vinavyoheshimika duniani) ni Maprofesa UCHWARA! Tatizo la nchi hii ni kubwa hadi mkuu wetu hajua tutaanzia wapi. Kwa uwazi kabisa nasema hii ni AIBU KUU!
Mtatiro J

<meta name="propeller" content="2fc3eb0573476ec843ed3750cc0fd772" />

Saturday, July 2, 2016

 Tamko la RC Makonda kuhusu mashoga waliopo jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza vita na makaka poa (mashoga) na madada poa (makahaba) walioko jijini Dar es Salaam kuwa utaendeshwa msako mkali wa kuwaondoa.

Mkuu wa Mkoa huyo aliyasema hayo kufuatia hali ya vitendo hivyo visiyokubalika na jamii kuzidi kushamiri na kuwa kuna hatari kubwa ya watoto wadogo kuiga vitendo hivyo vinavyoleta picha mbaya kwani ni kinyume na maadili ya mtanzania.

Aidha alisema hawezi kuifumbia macho hali hii kwani inamomonyoa maadali ya jamii na kuwa yuko tayari kulivalia njuga suala hili ili kuhakikisha anawamaliza wote mkoani

Sakati hili la ushoga na ukahaba limeibuka siku za hivi karibuni baada ya kituo cha televisheni cha Clouds Tv kumhoji shoga mmoja ambapo jamii ilipinga kitendo hicho na kuona kama walikuwa wakiuhalalisha ushoga na kuaminisha jamii kuwa ni kitu kizuri.

Friday, July 1, 2016

Nilivyofanya Bonge la Sherehe Baada ya Mke Wangu Kufukuzwa Kazi


Huyu mke nilimuoa akiwa hana kitu, kwa bahati alitafutiwa kazi na ndugu yake kwenye kampuni moja ya simu akawa analipwa kama milioni 3 kwa mwezi fasheni na yeye yeye na fasheni vipodozi kila aina,handbag na nywele za laki mbili ndio mshahara wake ukawa unaishia huko mimi mshahara wangu hauzidi laki sita,nilifanyishwa vituko vyote ndani ya nyumba ,manyanyaso yote ,hapiki hafui,hafanyi chochote ndoa ikawa inaelekea kuvunjika.

Nikaenda mahakamani kuprocess talaka wakasema mpaka nianzie baraza la usuluhishi la kata au kanisani,nikaamua kwenda kanisa tulilofungia ndoa tukaitwa kwa Baba Paroko for hearing sijui mediation sijui arbitration sijui mie nikatinga kwa bajaj ya kukodi nimepaukaaa yeye akaja na RAV4 .
Baba Paroko alivyotusikiliza akaaniita pembeni akasema kijana hapa nadhani hata tukiomba na kukariri mistari yote ya biblia plus mapambio yote ndoa yako haitarudi kama mwanzo pambana utafute hela ,huyu ni mchaga katumwa pesa mjini

Nilisali sana nikasugua goti nikamuomba Mungu mara mambo yangu yakakaa sawa mshahara ukawa mara mbili plus marupurupu anagalau . baada ya miezi miwili sina hili wala lile mara simu yangu nilishangaa mke wangu kunipigia mchana ,tumeachishwa kazi kmpuni imeuzwa,hureeeeee niliruka ruka kwa furaha sana nikapigia simu washikaji tukaenda kunywa bia na nyama choma mpaka saa sita usiku kabla polisi na makonda hawajatuvamia nilijua ile kazi ndio inaniharibia ndoa na aliipata kibahati hawezi tena kupata kazi kama ile.

Hela yote ya NSSF akajaribu kufanya kila biashara biashara zikabuma mtaji ukakata alijifanya hajui kupika sasa anapika kuliko hata wapishi wa Kempinski,alijifanya sijui hawezi kufua sasa anafua kuliko dobi ,kitandani alijifanya mvivu sasa yuko vizuri kuliko wacheza shoo wa fally ipupa ,RAV4 imepaki tu muda wote ananilelea watoto kwa nini nisimshukuru Mungu

Funzo:
Wanawake Msijisahau sana pale mnapokuwa vizuri kifedha zaidi ya mume