Tuesday, June 28, 2016

Yanga mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara wamepoteza mechi yao ya  pili katika kundi A la kombe la shirikisho Tanzania bara.Yanga ambao walionyesha kandanda safi leo uwanja wa Taifa walikubali kichapo hicho huku wakiwa na wachezaji wao wote wa kulipwa pamoja na mchezaji wao waliomsajili hivi karibuni Obrey Cholla Chirwa kwa gharama kubwa.

    Ushindi huo umewafanya TP Mazembe kufikisha point 6 nakuwa vinara kwenye kundi lao hilo,iliwachukuwa dakika 74 kuweza kupata bao lao hilo moja na la ushindi ambako mlinzi wao raia wa Congo kwa jina Merveille Bope akiifungia Mazembe .Yanga sasa inashika mkia katika kundi hilo.
                                                                                                                                                                       

Hifazi kubwa zaidi ya Gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania.

Tanzania ni miongoni mwa mataifa chache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi.
Na baada ya kugunduliwa kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania.

Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.

Ugunduzi huo umefanyika katika eneo la bonde la ufa la Tanzania.
Katika taarifa kwa wanahabri huko Japan, watafiti hao wanasema kuwa uhaba wa gesi hiyo kote duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari ambao wanatumia gesi hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama MRI scanners, mbali na kutumika katika mitambo ya kinyuklia miongoni mwa sekta zingine nyingi za kawi na teknolojia.

Kabla ugunduzi huo watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo baridi ifikapo mwaka wa 2035.

Mnamo mwaka wa 2010 Mwanfisikia mshindi wa tuzo la Nobel Robert Richardson alikuwa ametabiri kumalizika kabisa kwa gesi hiyo.

Ukosefu huo ulikuwa umesababisha wataalamu kuhimiza kutungwa kwa sheria itakayopunguza matumizi yake katika bidhaa zisizo za dharura kama vile kwenye vibofu kutokana na hali ya kuwa gesi hiyo ya Helium ni nyepesi kuliko ile ya Oxygen.

''Gesi tuliyoipata huko Tanzania inaweza kujaza silinda za gesi milioni moja nukta mbili za mashine za MRI'' alisema Chris Ballentine kutoka chuo kikuu cha Oxford.
Uwanja wa TAIFA wa furika milango yafungwa saa tano baada ya watu kujaa..
TFF imeeleza kuwa milango ya uwanja huo ilifungwa  saa tano asubuhi kutokana na wingi wa mashabiki waliojitokeza uwanjani hapo na kuingia moja kwa moja uwanjani.

Hadi kufikia saa 11:53 asubuhi, mashabiki waliokuwa nje ya uwanja hawakuruhusiwa kuingia ndani kufuatia majukwaa kufurika mashabiki, nafasi ya kuingia uwanjani imebaki kwa watu maalumu na Wanahabari pekee ambao wanaingilia mlango mkubwa wa Uwanja wa Taifa wakati ile mingine ikiwa imefungwa.

Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas alisema walilazimika kufungua milango ya uwanjani mapema tofauti na walivyoeleza awali kutokana na mashabiki kufurika uwanjani kuanzia saa tatu asubuhi.
"Mashabiki walianza kumiminika uwanjani kuanzia saa tatu, hatukuwa na namna zaidi ya kufungua milango ya uwanja muda huo ili kuwapa fursa ya kuingia na kupunguza msongamano," alisema Lucas.
Msinifananishe na mal*ya ambao hawajawai kwenda labor kujifungua...Zari
Nani amemchokoza Zari? Kwasababu kwa kile alichokipost kwenye mtandao wa Snapchat inaonekana ameguswa pabaya na amemind!

Najua unajiuliza kwanini hajapost Instagram – ni kwasababu kwa alichokiandika, povu lake lingekuwa la haja! Snapchat ya kishua, mastaa wako huru kusema chochote na hakuna povu kama mitandao mingine. Amesema nini?

“Na wengine acheni kunifananisha na mal*ya ambao hawajawahi kwenda labour,” aliandika. “Mtoto mmoja tu kwenye labour na watakaonekana kama tikiti maji lililopasuliwa. Acheni!”

“Nikiwa na miaka 35 na watoto wanne, badi mimi ni mrembo mno kunifananisha, naomba.”
Afariki baada ya kuchapwa na wazee wa kimila.
Picha ya Tukio jingine
Mtu mmoja mkazi wa Kijiji cha Kandashi, wilayani Siha, mkoani Kilimanjaro, Abedi Akyo (53), amefariki dunia baada ya kudaiwa kuchapwa viboko na wazee wa kimila kwa tuhuma ya kujihusisha na wizi wa kuku.

Akielezea mazingira ya kifo hicho, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilfred Mutafungwa amedai kuwa Akyo alichapwa viboko 70 na wazee hao wa kimila wa Kimeru na Kimasai.

Mutafungwa amesema watuhumiwa watafikishwa mahakamani baada ya kuwasiliana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mwezi uliopita  wakazi wa Kata ya Karansi wilayani hapa  walitoa uamuzi kuwa wanawake watakaovaa sketi fupi na vijana watakaovalia suruali chini ya kiuno, wataadhibiwa kwa kuchapwa viboko 60 hadi 70.
Utajiri wa Diamond umefikia shilingi bilioni 8.6
Kumekuwepo na tetesi nyingi kuhusu utajiri wa Diamond umefikia kiasi gani. Hilo ni swali ambalo hajawahi kulijibu kwa uhakika zaidi ya kutoa tu hints na kuwaacha wanaouliza kubaki na majibu yao wenyewe vichwani.

Lakini kupitia kipindi maalum cha kituo cha runinga cha E!TV, E Vip kilichorushwa Jumapili ya June 26, tunaweza kusema walau kwa uhakika staa huyo ana utajiri mkubwa kiasi gani. Diamond ana utajiri wa dola milioni 4 za Kimarekani ambao kwa shilingi ya Tanzania ni zaidi ya bilioni 8.6.

Si kitu kinachoshangaza tena kwa Diamond kutokana na hatua aliyofikia akiwa msanii anayelipwa fedha nyingi zaidi Tanzania kwa sasa. Fedha zake nyingi zinatokana na show zake zisizokauka za ndani na nje ya nchi, mikataba ya ubalozi na matangazo kutoka makampuni kama Vodacom, Cocacola, DSTV na Red Gold. Hivi karibuni alipata deal jingine la kutangaza huduma ya taxi ya Uber.

Pia amekuwa akiingiza fedha nyingi kupitia biashara ya nyimbo zake hasa miito ya simu, malipo ya mirabaha kutoka nchi za jirani kama Kenya bila kusahau biashara za mtandaoni zikiwemo Youtube.

Uwekezaji wake kwenye label ya WCB ni kitu kingine kikubwa ambacho kitaanza kumuingizia fedha nyingi siku za usoni. Hadi sasa amesaini wasanii wanne wakiwemo Rich Mavoko, Raymond, Harmonize na dada yake Queen Darleen.

Lakini pia staa huyo anafahamika kwa kuwekeza zaidi fedha kwenye ardhi na nyumba huku akidaiwa kumiliki maeneo mengi jijini Dar es Salaam.

Uwoya amtia majaribuni Richie
Irene Uwoya na Richie.
WAKATI Waislam wakiwa kwenye Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya juzikati alimtia majaribuni msanii mwenzake Single Mtambalike ‘Richie’ walipokuwa kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar kulikokuwa na harusi ya mdogo wake Steve Mengere ‘Steve Nyerere’, Happy Mengere.

Kwenye ‘mnuso’ huo, Uwoya aliyekuwa amevalia kivazi kilichoacha mapaja yake wazi, alionekana mara kadhaa akimkumbatia Richie na hata paparazi wetu alipotaka kuwafutoa picha, staa huyo alimshika kimahaba na kuwaacha watu wakinong’ona chinichini.

“Uwoya hivi haoni anamtia mwenzake majaribuni? Na Mwezi Mtukufu huu analazimisha kupiga naye picha ya kumkumbatia, ila hawa wasanii wamezoeana sana,” alisema mmoja wa waalikwa aliyekuwa karibu na mastaa.

Paparazi wetu aliyekuwa eneo la tukio alipojaribu kuwakaribia na kumuuliza Uwoya kulikoni anamfanyia mwenzake vituko alisema, alijisahau kuwa Richie yupo kwenye Mwezi Mtukufu ila alipiga picha hiyo kama pozi la kawaida tu na wala hakuwa na nia mbaya
Lulu Michael kushtakiwa kwa kosa la kimtandao...
Dar es Salaam: Mwigizaji wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ yupo mbioni kupambana na mkono wa sheria kufuatia kumvurumishia matusi mwandishi wa habari wa Global Publishers baada ya kumuuliza swali lililotaka ufafanuzi wake ikiwa ni siku chache tangu alipofanya hivyo kwa mwandishi mwingine wa kampuni hiyo.

Ishu hiyo ilitokea Ijumaa iliyopita ambapo paparazi alimtwangia simu ya mkononi Lulu na kumuuliza kuhusu kuwepo kwa madai kwamba, yeye ni mjamzito na amekuwa akishinda ndani kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, msanii huyo kwa vile sasa ni mama kijacho, amekuwa nadra kuonekana sehemu za hadhara kwa kuwa hataki watu wajue kwa kuwahofia wabaya wake.
“Ndo’ maana sasa kumuona Lulu waziwazi ni ngumu sana, naona yeye na aliyempa mimba (hakumtaja) wamepanga hivyo. Si unajua wambeya wengi, nadhani anahofia macho ya watu wenye vijiba vya roho na wale washirikina, wakimuona isije mimba ikachoropoka kabla ya wakati,” kilisema chanzo hicho.

Sasa kufuatia madai hayo, ilibidi paparazi amtafute Lulu mwenyewe ili kumsikia. Ni suala la kuweka mizani ya habari sawa kwa mujibu wa maadili ya taaluma, kwamba, mtu anapodaiwa kwa habari, lazima apewe nafasi ya kufafanua au kujitetea. Ni haki ya msingi kabisa.
Lakini cha ajabu, Lulu alipopatikana hewani na kusomewa madai hayo, hata kabla paparazi hajafika mwisho, alikuja juu huku akimwaga matusi kwa paparazi:

“Wewe … (jina la mwandishi), sitaki uniulize maswali ya ….. (tusi). Naomba usitake tukoseane heshima tukaonana wabaya jua nakuheshimu sitaki nikutukane halafu tufikikishane mahakamani laivu. Hayo mambo nenda kawaulize haohao waliyokwambia…(tusi).
Paparazi: Mimi nimeagizwa na mabosi wangu nikuulize…
Lulu: (akadakia) wewe na hao mabosi zako….(tusi).

KUTOKA KWA MHARIRI
Kufuatia matusi yake hayo ambayo hayaandikiki gazetini, paparazi wetu alikwenda Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ili kulalamika ambapo mtumishi mmoja alimtaka kurudi Jumatatu (leo) kwa ajili ya kuandika maelezo kwenye kitabu cha malalamiko tayari kwa hatua zaidi.
Kwa Lulu ambaye kujulikana kwake na kuwa staa kulitokana na habari zake kuandikwa kwenye magazeti pendwa, hasa ya Global, amekuwa na tabia ya kuwatukana mara kwa mara mapaparazi wetu huku akitishia kuwapeleka mahakamani. Hufanya hivi kila anapotakiwa kutolea majibu au ufafanuzi habari inayomhusu.

KOSA LA KIMTANDAO
Katika makosa ya mtandao yaliyoanza kufanya kazi nchini Septemba Mosi, 2015, kuna kifungu kinasema; Epuka kumtusi, kumkebehi mtu kutokana na utaifa wake, rangi yake, kabila au dini yake.

TUJIKUMBUSHE
Ishu ya Lulu kuwatusi waandishi wetu si mara ya kwanza kwani mwandishi mwingine wa gazeti hili alilalamika kujibiwa kwa karaha na msanii huyo alipotaka ufafanuzi wa jambo fulani

TP Mazembe watua dar na mashabiki kama 500 kuikabili Yanga hapo kesho.

Kuelekea katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaopigwa kesho Jumanne saa 10:00 jioni, uongozi wa Klabu ya Yanga umesema kuwa wanatarajia kuwapokea zaidi ya mashabiki mia tano wa TP Mazembe ambao watakuwepo uwanjani kuishangilia timu yao.



Licha ya Yanga kutangaza kuwa mchezo huo  utakuwa ni bure ambapo unatarajia kufanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro amesema tayari wameshapokea tarifa kutoka kwa wapinzani wao hao kuwa watakuwa na mashabiki zaidi ya mia tano kutoka nchini DR Congo kwa ajili ya kuisapoti timu yao.


“Tumepokea taarifa kutoka kwa wenzetu wa TP Mazembe ambao wametueleza kuwa kuna msafara mashabiki wao wapatao mia tano wapo njiani, wanakuja kwa ajili ya kuisapoti timu yao katika mchezo wa kesho,” alisema Muro na kuongeza:

     “Sasa niwaombe tu mashabiki wa Yanga na Watanzania kwa jumla wajitokeze kwa wingi   uwanjani ili tuwazidi hao wa kwao mia tano.”


Mashabiki wa TP Mazembe wanajulikana kwa kuwa na nguvu kubwa ya kushangilia bila kujali wakiwa nyumbani au ugenini, ambapo walipowahi kuja nchini miaka kadhaa iliyopita kucheza dhidi ya Simba walikuwa na kikundi cha ngoma kilichokuwa kivutio kwa mashabiki wengi nchini.